URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la elimu Tanzania
       *****************************************************
       #Post#: 1391--------------------------------------------------
       SHULE BORA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2014
   DIR By: mando
       Date: February 15, 2015, 9:52 am
       ---------------------------------------------------------
       SHULE BINAFSI ZATESA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE
  HTML http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/2624432/highRes/945935/-/maxw/600/-/beu9utz/-/bora.jpg
       Ufaulu katika matokeo ya mtihani wa kidato cha nne umeongezeka
       kwa asilimia 10, chini kidogo ya viwango vya Matokeo Makubwa
       Sasa (BRN), lakini shule za Serikali za vipaji maalumu, kongwe
       na za seminari zimeendelea kuporomoka. Katika matokeo hayo,
       Shule ya Sekondari ya Kaizirege ya mkoani Kagera, iliyoanzishwa
       mwaka 2010, ndiyo imekuwa kinara ikiwa ni mwendelezo wa
       mafanikio baada ya mwaka jana kushika nafasi hiyo lakini kwa
       upande wa shule zenye watahiniwa chini ya 40. Shule iliyoshika
       mkia ni Manolo iliyopo Tanga, mkoa ambao umetoa shule tano
       miongoni mwa shule zilizoshika nafasi 10 za mwisho. Matokeo hayo
       ni ya kwanza tangu kuanza kutumika kwa mfumo mpya wa upangaji wa
       Wastani kwa Kutumia Pointi (GPA) ambao unaonyesha shule zote 10
       za kwanza ni za binafsi. Akitangaza matokeo hayo jana jijini Dar
       es Salaam, Katibu Mtendaji wa Baraza la Mitihani la Taifa
       (Necta), Dk Charles Msonde alisema waliofaulu mtihani huo ni
       wanafunzi 196,805 sawa na asilimia 68.33 ya watahiniwa 288,247
       waliofanya mtihani huo, ikilinganishwa na 235,227, sawa na
       asilimia 58.25 ya waliofaulu mwaka 2013. Dk Msonde alisema
       wavulana waliofaulu ni 106,960 sawa na asilimia 69.85 na
       wasichana ni 89,845 sawa na asilimia 66.61. Kwa mujibu wa
       maelekezo ya BRN, ufaulu wa upande wa sekta ya elimu, ambayo
       ilipangiwa malengo tisa, ulipaswa uwe asilimia 70. Hata hivyo,
       pamoja na kuwa chini kidogo ( asilimia 1.7) kufikia wastani wa
       ufaulu kitaifa, Msonde alisema: “Tumejitahidi kwani ni asilimia
       kama moja na ushee ilibaki, walimu walifanya kazi nzuri na nina
       imani tutaifikia.” Alisema watahiniwa 297,365 waliandikishwa
       kufanya mtihani huo wakiwamo wasichana 139,400 sawa na asilimia
       46.88 na wavulana 157965 sawa na asilimia 53.12. Watahiniwa wa
       shule walikuwa 244,902 ikilinganishwa na watahiniwa 367,163
       walioandikishwa kufanya mtihani huo mwaka 2013. “Idadi ya
       watahiniwa wa shule walioandikishwa kufanya mtihani huo
       ilipungua kwa asilimia 33.3 ikilinganishwa na watahiniwa
       walioandikishwa mwaka 2013.” “Mwaka 2012 kati ya watahiniwa
       386,355 waliofanya mtihani wa kidato cha pili, watahiniwa
       136,243 walirudia kidato cha pili na watahiniwa 250,112
       waliendelea na kidato cha tatu ambao ndiyo waliosajiliwa kufanya
       mtihani wa kidato cha nne mwaka 2014,” alisema na kuongeza:
       “Kati ya watahiniwa 297,365 waliosajiliwa kufanya mtihani wa
       kidato cha nne 2014, watahiniwa 288,247 sawa na asilimia 96.93
       walifanya mtihani na watahiniwa 9,118 sawa na asilimia 3.07
       hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali.” Alisema
       watahiniwa wa shule, kati ya watahiniwa 244,902 waliosajiliwa
       watahiniwa 244,410 sawa na asilimia 98.17 walifanya mtihani
       ambao wasichana walikuwa ni 110,603 sawa na asilimia 98.13 na
       wavulana ni 129,807 sawa na asilimia 98.19. Watahiniwa 4,492
       sawa na asilimia 1.83 hawakufanya mtihani. Kwa upande wa
       watahiniwa wa kujitegemea, alisema kati ya watahiniwa 52,463
       waliosajiliwa, 47,837 ambao ni sawa na asilimia 91.18, walifanya
       mtihani na ambao hawakufanya ni 4,626 sawa na asilimia 8.82.
       Ufaulu wa masomo Dk Msonde alisema ufaulu wa watahiniwa wa shule
       katika masomo ya msingi umepanda kati ya asilimia 1.28 na 11.22
       ikilinganishwa na mwaka 2013. “Ufaulu wa juu kabisa ni ule wa
       somo la Kiswahili na asilimia 69.66 ya watahiniwa wote wa shule
       waliofanya somo hili wamefaulu na ufaulu wa chini kabisa ni ule
       wa somo la hisabati ambalo asilimia 19.58 ya watahiniwa wote
       waliofanya somo hili wamefaulu.” “Ufaulu katika masomo ya
       sayansi yaani fizikia, kemia na baiolojia umeendelea kuimarika
       kidogo kwa kulingana na ufaulu wa masomo hayo mwaka 2013,”
       alisema. Katika matokeo hayo, ufaulu wa kila somo na asilimia
       katika mabano ni Kiswahili (69.66), kemia (56.73), Kiingereza
       (55.10), baiolojia (48.30), fizikia (46.71), jiografia (37.96),
       uraia (37.70), historia (37.41), biashara (34.29), uhasibu
       (42.20) na hisabati (19.58). Matokeo yaliyozuiwa, kufutwa Dk
       Msonde alisema baraza limefuta matokeo ya watahiniwa 184
       waliobainika kufanya udanganyifu. Kati ya watahiniwa
       waliobainika kufanya udanganyifu, 128 ni wa kujitegemea na 56 ni
       watahiniwa wa shule. Alisema kati ya watahiniwa hao, 128
       wanatoka vituo viwili vya Kisesa mkoani Mwanza na Ubago visiwani
       Zanzibar, huku wengine 56 wakitoka shule mbalimbali. “Tumeagiza
       mamlaka husika kuwachukulia hatua za kinidhamu waliohusika
       katika vituo hivyo vya Kisesa na Ubago kwani udanganyifu
       uliofanyika ni karatasi moja ya kujibia mtihani imeandikwa na
       watu watatu tofauti jambo ambalo linaonyesha hakukuwa na
       umakini,” alisema. Shule kongwe na za vipaji hoi Shule za vipaji
       kama Ilboru, Mzumbe, Msalato, Kilakala, Tabora Boys, Kibaha na
       Tabora Girls na Shule kongwe zinazomilikiwa na Serikali kama
       Pugu, Zanaki, Bwiru Boys, Minaki, Azania na Jangwani, kwa mara
       nyingine zimeshindwa kufua dafu kwa shule za binafsi. Katika
       orodha ya shule 10 bora shule binafsi zilizotamba katika matokeo
       hayo ni Kaizirege (Kagera), Mwanza Alliance (Mwanza), Marian
       Boys (Pwani), St. Francis Girls (Mbeya), Abbey (Mtwara), Feza
       Girls (Dar es Salaam), Canossa (Dar es Salaam), Bethel Sabs
       Girls (Iringa), Marian Girls (Pwani) na Feza Boys (Dar es
       Salaam). Shule 10 za mwisho ni Manolo (Tanga), Chokocho (Pemba),
       Kwaluguru (Tanga), Relini (Dar es Salaam), Mashindei (Tanga),
       Njelekela Islamic Seminari (Kigoma), Vudee (Kilimanjaro), Mnazi
       (Tanga), Ruhembe (Morogoro) na Magoma (Tanga). Watahiniwa 10
       bora kitaifa Dk Msonde aliwataja wanafunzi 10 bora kitaifa kuwa
       ni Nyakaho Marungu (Baobab), Elton Jacob (Feza Boys), Samwel
       Adam (Marian Boys), Fainess Mwakisimba (St. Francis Girls),
       Mugisha Lukambuzi (Bendel Memorial), Paul Jijimya (Marian Boys),
       Angel Mcharo (St. Francis Girls), Atuganile Jimmy (Canossa),
       Jenifa Mcharo (St. Francis Girls) na Mahmoud Bakili (Feza Boys).
       Wasichana 10 bora kitaifa Katika matokeo hayo mwanafunzi bora
       kwa wasichana ni Nyakaho Marungu (Baobab), aliyefuatiwa na
       Fainess Mwakisisimba (St. Francis Girls), Angel Mcharo (St.
       Francis Girls), Atuganile Jimmy (Canossa), Jenifa Mcharo (St.
       Francis Girls), Levina Ndamugoba (Msalato), Veronica Wambura
       (Canossa), Sifaely Mtaita (St Maris Mazinde Juu), Catherine
       Ritte (St. Francis Girls) na Anastazia Kabelinde (Kaizerege).
       Wavulana 10 bora Dk Msonde alimtangaza kinara kwa wavulana kuwa
       ni Elton Jacob (Feza Boys) akifuatiwa na Samwel Adam (Marian
       Boys), Mugisha Lukambuzi (Bendel Memorial), Paul Jijimya (Marian
       Boys), Mahmoud Bakili (Feza Boys), Amani Andrea (Moshi
       Technical), Mahmoud Msangi, Elias Kalembo, Haji Gonga na Kelvin
       Sessan wote kutoka Feza Boys. CHANZO MWANANCHI.
       *****************************************************
       Page 1 of 1