URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la wanafunzi Tanzania (JUWATA)
       *****************************************************
       #Post#: 1348--------------------------------------------------
       Mabinti wanafunzi acheni kuwatega wavulana na wanaume
   DIR By: Trainer
       Date: February 8, 2015, 7:33 am
       ---------------------------------------------------------
       Leo wapendwa wanafunzi ningependa kuwashauri watoto wa kike
       yaani mabinti wasichana.
       Mara nyingi mmekuwa mkitetewa na kulindwa sana na vyombo
       mbalimbali vya kijamii. Lakini mnajua kuwa na nyie mnatakiwa
       kujisitiri vizuri ili msiwatege wanaume na hatimae waanze
       kuwasumbua kimapenzi.
       Mtoto wa kike anashonewa sketi ndefu na wazazi wake lakini
       akifika shuleni kama ni boding anapeleka ile sketi kwa fundi ili
       apunguze urefu au anaikunja kwa nyuma ili mapaja yaonekane
       vizuri upande wa nyuma . Sasa hapa unakuwa unategemea nini
       kitafuata?
       Kuwapa sketi ndefu ni kuwasaidia nyie msisumbuliwe na wanaume.
       Ni kweli kuna wanaume ambao wenyewe wakiona sketi ya mwanafunzi
       wanawaza kumtongoza mwanafunzi huyo, ila na nyie wasichana basi
       mjitahidi kutowashawishi wavulana ili wawatongoze.
       Tunajua mnaweka mitego hiyo ili wavulana au wanaume wawatongoze
       ili muanze kupata pesa za matumizi na chipsi kuku lakini mjue
       mwisho wake unaweza kuwa si mzuri. Utapewa mimba taaluma
       itashuka na unaweza usifikie ndoto zako za kimaendeleo.
       Kwa walionielewa nawashukuru wasionielewa wataelewa wakishapewa
       mimba na kutelekezwa.
       Una mchango wowote wewe mwanafunzi au mlezi au mzazi tujadili
       hapa Asante.
       *****************************************************
       Page 1 of 1