URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la wanafunzi Tanzania (JUWATA)
       *****************************************************
       #Post#: 1296--------------------------------------------------
       Mambo 5 yatakayokusaidia kufaulu mtihani wako
   DIR By: Trainer
       Date: February 3, 2015, 1:34 pm
       ---------------------------------------------------------
       Mwanafunzi jifunze mambo 5 yatakayokusaidia kufaulu mitihani
       yako hapo shuleni unaposoma hata kama hakuna walimu wa kutosha
       au vitendea kazi vya kutosha
       Nitakupa siri ya kwanini wanafunzi wanaosoma shule za seminary
       huwa wanafaulu vizuri zaidi ukilinganisha na shule zisizo za
       seminary au shule zisizo za international.
       Hakuna kitu cha pekee kilichopo huko saint somebody ambacho
       kinawafanya wanafunzi hao wafaulu vizuri kwa wastai mzuri wa
       darasa zima.
       Siri ndiyo hii Yajue mambo matano yatakayokufanya ufaulu mtihani
       wako hata kama upo kwenye mazingira magumu za kujisomea.
       1.
  HTML http://www.chatguest.com
       Heshima na Nidhamu. Waheshimu walimu
       wako hii itakufanya uwe rafiki wa walimu hao hivyo kutokana na
       urafiki huo walimu hawatapenda rafiki yako afeli hata siku moja.
       Heshima kwa wanafunzi wenzio. Usijikweze na kujiona labda wewe
       ndiye unayejua sana hapo shuleni au wewe ndiye mwenye pesa
       nyingi kati ya wanafunzi wote. Ukiwaheshimu wanafunzi wenzio nao
       watakuona wa maana na hawatakutenga kwa chochote
       kitakachokusaidia kufaulu mitihani yako.
       Nidhamu kwa ujumla kufuata ratiba kama ilivyoandaliwa na shule.
       Siku ya kuripoti tarehe 10 mwezi wa kwaza 2015 saa kumi kamili
       kweli muda huo uwe shuleni umeshafika acha misemo ya Aaa mimi
       nitavuta wiki mbili kwasababu wiki ya kwanza yote na ya pili
       walimu hawataanza kuingia madarasani. Elimu sio ile ya kwenye
       makaratasi tu kama unavyofikiri, Stadi za kazi nazo ni muhimu
       kama wiki ya kwanza umezoea huwa mnafanya usafi wa mazingira
       basi hakikisha na wewe unashiriki kikamilifu. Hii itakusaidia
       kuondo hofu ya kuchelewa kuripoti na kupewa azabu zisizo za
       lazima Pia unajifunza kuja kujitegemea baadae hata usipofanikiwa
       kuajiriwa kwenye kazi zinazotaka cheti kina alama gani badala ya
       mwajiriwa anauwezo gani.
       2.
  HTML http://www.chatguest.com
       Saidia wenzio kitaaluma hata katika
       mahitaji mengine ambayo unaona mtu fulani anauhitaji na wewe
       unaweza kumsaidia. Wengi wanakuwa wachoyo wa kuwasaidia wengine
       kitaaluma. Kama unajua hesabu za log vizuri na unatambua mtu
       fulani haziwezi kabisa hesabu hizo basi mwite mwambie fulani
       nataka leo nikufundishe hesabu za log mpaka uzielewe ni rahisi
       sana. Sasa utashangaa faida utakayoipata kwanza ukimfundisha
       mwezio wewe ndiyo ule ujuzi unakukaa zaidi ukiwa kwenye mtihani
       utakumbuka siku ile uvyokuwa unamfundisha maria tabu mpaka
       akaelewa kwahiyo utakuta unapata alama nzuri zaidi kwenye
       mtihani wako.
       Faida nyingine utapata vitini vya masomo mengine na past paper
       ambazo hujawahi kuziona wala kuwa nazo hii ni kutokana na tabia
       ya watu ambao wanakuwa na shida ya kuelewa masomo fulani huwa
       wanatafuta material kwa hali na mali hivyo watu kama hao
       ukioneshania ya kuwasaidia watakuona wa mana na kushare pamoja
       nawe material walionayo. Hutahangaika kununua vitabu au vitini
       vyote utavipata kwa marafiki kama una moyo mzuri wa kuwasaidia.
       Lasivyo hawa watu watafungia vitini kwenye matranka yao na
       hatimaye wote hamfaulu kwa kiwango kikubwa kama shule za saint
       somebody
       3. Jiwekee malengo ya kufaulu; Hata kama unaona wastani wa test
       unazofanya haulizishi wewe weka malengo kuwa kama imetoka
       umefeli basi uwe umefeli kwa alama B
  HTML http://www.chatguest.com
       ukiweka mengo hayo basi ikitokea
       umefeli utafeli kwa alama C ambayo ni credit na itakuwezesha
       kunedelea na ngazi za juu kama wengine wenye alama A.Usikate
       taamaa hata kidogo, Unaweza kuta maajabu somo unaloliogopa sana
       ndilo litakalokutoa.
       4. Acha ulimbukeni. Ushalobalo, Usista du, Mapenzi shuleni hivyo
       vyote utavifanya ukisha maliza masomo yako. Kwanza ukishamaliza
       masomo. Ukianza vitu hivyo shueni taaluma itashuka tu.
       5. Fanya mazoezi mara nyingi uwezavyo hapa sizungumzii mpira au
       mazoezi ya kukimbia hapana nazungumzia kurudia rudia zoezi la
       somo fulani. Mfano kama umejifunza definition ya what is biology
       basi andika na kuikariri defintion hiyo hata mara miamoja.
       Nimemkumbuka mwalimu moja mhindi alikuwa akisahihisha somo lake
       akakuta umekosea neno moja tu kwenye sentensensi hiyo anakuagiza
       uandika sentensi hiyo mara elfu moja kisha umpelekee asahihishe
       tena sasa mwenzangu karatasi za kuandika hiyo sentensi mara elfu
       moja gharama yake si umeshapunguza pesa za kununulia andazi la
       kutafunia na uji uliowekwa chumvi ha ha ha ha Ila alikuwa
       anasaidia sababu ukirudia rudia kitu huwezi kukisahau. Wazungu
       wanasema "Practice makes perfect"
       Naomba kwa leo tuishie hapa kama kuna typing error
  HTML http://www.chatguest.com
       popote hapo juu basi uniwie radhi hii
       nikutakana na muda mfupi niliopata sikuweza kusahihisha
       maandishi hayo.
       Safari ijayo nitakupa mambo muhimu  5 ya kufuata ukiwa kwenye
       chumba cha mtihani hata kama hukujiandaa vizuri kwa mtihani huo
       bado utafaulu tu, na usipofuata mambo hayo hata kama ulijiandaa
       vizuri bado utafeli tu au hutafaulu kwa kiwango kikubwa
       Kama uandhani makala hii inaumuhimu kwa mwanafuzi basi like na
       share huko facebook twitter na kwingineko
       Una swali, shukani au nyongeza bonyeza "repy" hapo juu kulia.
       *****************************************************
       Page 1 of 1