URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la elimu Tanzania
       *****************************************************
       #Post#: 1177--------------------------------------------------
       AJUZA WA MIAKA 90 ANASOMA DARASA LA NNE Kweli elimu haina mwisho
   DIR By: udaku
       Date: January 23, 2015, 5:30 am
       ---------------------------------------------------------
       HAYA SI MAAJABU? AJUZA WA MIAKA 90 ANASOMA DARASA LA NNE
  HTML http://ichef.bbci.co.uk/news/ws/660/amz/worldservice/live/assets/images/2015/01/23/150123014307_gogo_512x288_bbc_nocredit.jpg
       Akiwa na umri wa miaka 90 mwanamke wa Kenya ambaye anahudhuria
       masomo akiwa na wajukuu zake wapatao sita inaaminika ndiye
       mwanafunzi mzee zaidi anayesoma shule ya msingi duniani. Akiwa
       ameketi dawati la mbele kabisa darasani ,yuko darasa la tano na
       amevalia nguo za shule , Priscilla Gogo Sitienei anamsikiliza
       mwalimu anayefundisha kwa makini hukua akiandika majina ya
       wanyama kwa kiingereza kwenye daftari lake. Prissilla alijiunga
       na shule hii ya Leaders Vision Preparatory School miaka mitano
       iliyopita lakini pia aliwahi kuwahudumia wakaazi wa kijiji chake
       cha Ndalat kilichoko kwenye bonde la ufa kama mkunga miaka
       sitini na mitano iliyopita. Darasani Priscilla anawasaidia
       wengine wafanye vyema ambao wana umri kati ya miaka 10 hadi 14
       na mar azote huwaambia ujumbe wake hasa mabinti kuwa elimu ndiyo
       urithi wao. Priscilla anajulikana kama Gogo maana yake bibi
       katika lugha ya jamii ya wakalenjini,anasefurahia masomo akiwa
       na umri wa miaka 90 katika umri huo anajua kuandika na kusoma
       pia fursa aliyoikosa alipokuwa mdogo. Lugha ambayo Priscilla
       anajiona yuko huru kuitumia ni lugha mama kwake ki Kalenjin
       kuliko kiingereza,pindi anapotakiwa kujieleza kwanini aliamua
       kujiunga na shule katika umri wake. Sababu kubwa ambayo amekuwa
       akiitoa,ni ajue kusoma ili amudu kusoma bibilia,lakini pia kwa
       umri wake anataka awahamasishe watoto kupata elimu,kwani
       anawaona watoto wengi wakiwa hawako shuleni na watoto hao wana
       watoto. Gogo apitapo mitaani haoni shida kukabiliana na watoto
       ambao hawako shuleni katika muda wa masomo na kuwauliza kwanini
       hawako shuleni. Gogo anasema watoto hao humjibu kwamba hawaendi
       shule kwakuwa umri wao ni mkubwa,name huwaambia mimi ni mkubwa
       sana kwenu lakini niko shuleni hivyo nanyi jiungeni na shule.
       Kikubwa kinachomuumiza Gogo ni kuwaona watoto wengi waliopoteza
       muelekeo,wengi wao hawana baba na wanazurura hovyo mitaani,bila
       msaada wowote.kutokana na hali hiyo nataka kuwahamsisha waende
       shuleni.
       Chazo BBC
       *****************************************************
       Page 1 of 1