DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
habari
HTML https://habari.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: Sports and entertainments
*****************************************************
#Post#: 1152--------------------------------------------------
Hapatoshi leo England, Man City vs Arsenal
DIR By: mastory
Date: January 18, 2015, 12:47 am
---------------------------------------------------------
HTML http://3.bp.blogspot.com/-Yjb2duwyWi8/VLtQsEvyqeI/AAAAAAAAOXI/-YN9Rz3m_2E/s1600/EPL.jpg
KIVUMBI cha Ligi Kuu ya England kinatarajiwa kuendelea leo kwa
mechi mbili likiwamo linalovuta hisia za wengi litakalochezwa
kwenye uwanja wa Etihad mjini Manchester kati ya wenyeji
Manchester City dhidi ya Arsenal.
Pambano jingine la leo litazikutanisha timu za West Ham Utd
watakaokuwa nyumbani kuwakaribisha Hull City katika uwanja wa
Boleyn.
Mabingwa watetezi Manchester City wataikaribisha Arsenal
wakitoka kulazimishwa sare katika mechi yao ya mwisho, ilihali
Arsenal wakitoka kupata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya
Stoke City.
Ingawa Arsenal itakosa huduma za beki wake Mathieu Debuchy
aliyeumia bega katika mechi yao iliyopita sambamba na kuwakosa
wakali wengine ambao ni majeruhi kama ambavyo watetezi Man City
watakavyokosa huduma za wakali wake akiwamo Yaya Toure na
Wlifried Bony waliopo Afrika kwa sasa..
City itakuwa ikisaka ushindi nyumbani kuweza kuendelea kuwabana
Chelsea wanaoongoza msimamo wa ligi hiyo wakati wao wakiwa wapo
nafasi ya pili.
Watetezi hao wana pointi 47 wakati wapinzani wao Arsenal wakiwa
na pointi 36 wakishika nafasi ya tano.
Ligi hiyo itaendelea kesho kwa pambano moja tu
litakalozikutanisha timu za Everton dhidi ya West Bromwich
Albion mechi itakayochezwa kwenye uwanja wa Goodson Park.
credit micharazomitupu blog
*****************************************************
Page 1 of 1