DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
habari
HTML https://habari.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: Jukwaa la elimu Tanzania
*****************************************************
#Post#: 1017--------------------------------------------------
Elimu ya Sekondari itakuwa BURE kuanzia 2016 - Jakaya Kikwete
DIR By: udaku
Date: January 1, 2015, 12:16 am
---------------------------------------------------------
HTML http://2.bp.blogspot.com/-d_blVTw_Bmo/VKThEQXhIRI/AAAAAAAAl0U/VeYroLLkico/s1600/jk...jpg
Katika Salaam za Mwaka Mpya Kutoka kwa Rais Jakaya kikwete
Amegusia Swala la elimu na Kusema kuhusu Elimu ya Secondary
Mwaka ujao itakuwa ni Bure.
Nanukuu kama Ifuatavyo:
'Sera Mpya ya Elimu na Mafunzo
Ndugu wananchi;
Mafanikio mengine tuliyopata mwaka huu ni kukamilika kwa Sera ya
Elimu na Mafunzo ya mwaka 2014. Hii ni hatua muhimu sana katika
maendeleo ya elimu nchini hakuna badala yake. Sera mpya inalenga
kuinua ubora wa elimu na mafunzo na kuweka mifumo na taratibu
zitakazowezesha Watanzania wengi zaidi kupata fursa za elimu
iliyo bora na inayolinga na wakati tulionao. Jambo jipya sana na
la kihistoria katika Sera mpya ya Elimu ni dhamira ya Serikali
ya kuondoa ada katika elimu ya sekondari kuanzia mwaka 2016.
Mpaka sasa hatuna ada kwenye shule za msingi, sasa wakati
umefika kufanya hivyo pia kwa elimu ya sekondari. Kwa mujibu wa
maelezo hayo ya Sera, nimekwishatoa maagizo kwa Wizara ya Elimu
na Mafunzo ya Ufundi, Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa, Wizara ya Fedha na Tume ya Mipango kuanza kutafakari
namna jambo hilo litakavyotekelezwa.' Jakaya Kikwete"
Maoni yako kama mdau wa elimu hii inawezekana? Itakuwa bure
kweli au michango kibao?
*****************************************************
Page 1 of 1