DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
habari
HTML https://habari.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: Makala Bora
*****************************************************
#Post#: 3307--------------------------------------------------
MAKALA:MBINU ZA KUTUMIA ILI KUJIINGIZIA KIPATO KUPITIA BLOG NA
KUFIKIA MALENGO YAKO.
DIR By: Godfrey Mtega
Date: October 29, 2016, 8:04 am
---------------------------------------------------------
KARIBU SANA MSOMAJI WA MAKALA MBALIMBALI KATIKA BLOG YETU(MTEGA
BLOG)
MATUMIZI YA BLOG
1.KUWEKA HABARI NA TAARIFA MBALAMBALI.
Unaweza kutumia blog yako kuweka au kutangaza habari mbalimbali
za kikanda,kitaifa au hata za kimataifa.Habari kwa
maandishi,Habari kwa Picha na Habari kwa Sauti na Habari kwa
Video,Chaguo ni lako.
2.KUWEKA TAARIFA ZAKO BINAFSI
Unaweza kutumia BLOG kutunzia taarifa zako mbalambali kama vile
matukia\o yako ya kila siku,taarifa zako za nyumbani n.k
ANGALIZO:KAMA UNATAKA UWEKE TAARIFA ZA SIRI IWEKE BLOG YAKO
KATIKA PRIVATE,Baada ya kufanya hivyo hakuna mtu yeyote
atakayeweza kuona taarifa zako hata kama akaingia katika BLOG
YAKO.
3.Kutangaza biashara yako
NDIO, Kama una biashara yako na unataka kuinadi kupitia blog
basi inawezekana kabisa hapa kuna mbinu zinazohitajika ili uweze
kufanikiwa katika hili.Lugha ya Mvuto,Utumiaji mzuri wa
Picha,kuwa Mbunifu na jifunze jinsi ya kuongea na wateja.Toa ofa
na mengineyo.
4.KUTUMIA BLOG KWA AJILI YA MAWASILIANO KATIKA KAMPUNI
Kivipi, unaweza kuitumia blog yako kwa ajili ya mawasiliano ya
kampuni au Shirika mara nyingi blog za aina hii huwa zinwekewa
password hivyo Mtu asiyehusika hawezi kuingia.Hata wewe unaweza
kufanya pia.
5.Kutumia Blog katika Taasisi Mbalimbali
Unaweza pia Kuitumia Blog katika taasisi mbalimbali kama vile
Shule,Vyuo,Taasisi za kidini na hata Vikundi mbalimbali.Blog
itasaidia kurahisisha Mawasiliano.Kwa mfano Blog ya Shule
inaweza KUTUMIKA kuweka taarifa mbalimbali na matukio ya
Shule/Chuo kama vile Ratiba ya Vikao,Ratiba za Mitihani na
mengineyo.Blog ya shule na Chuo pia inaweza kutumika kuweka
JOINING INSTRUCTIONS(Hii ni barua inayotoa mwongozo wa MAELEKEZO
Y KUJIUNGA NA CHUO AU SHULE HUSIKA) Kumekuwa na ugumu wa
kupatikana kwa barua hizi na hivyo kuwafanya wanafunzi MUDA
MWINGINE, kusafiri umbali mrefu kwenda shuleChuo kuchukua
JOINING INSTRUCTIONS LETTER,BLOG INAMALIZA TATIZO HILI.
TUNAKUTENGENEZEA BLOG KWA GHARAMA NAFUU KUANZIA TZS 10,000/= TU.
TUPIGIE 0758297744.
ZIFUATAZO NI NJIA AMBAZO UNAWEZA KUZITUMIA KUJIINGIZIA KIPATO
KWA KUPITIA BLOG.
Hii ni sehemu muhimu ambayo karibu kila anayefungua blog anataka
afahamu jinsi gani anaweza kuingiza kipato kwa kupitia
blog.Swali linakuja je ni kweli mtu unaweza ukaingiza fedha kwa
kupitia blog? Jibu ni NDIO unaweza kuingiza kipato kwa kupitia
blog.Kabla ya yote unatakiwa ufahamu kuwa fedha ni thamani na
thamani yoyote haipatikani pasipo kuifanyia kazi,hivyo kuingiza
fedha kupitia blog vivo hivyo inahitaji ujitoe kwa kweli.Fahamu
pia kuwa inahitaji muda hadi uweze kuingiza kipato kupitia
blog.Urefu wa muda unatofautiana kuna ambao wanaanza kjiingizia
kipato ndani ya siku kadhaa wengine miezi kadhaa na wengine
inafikia hadi mwaka au zaidi.Yote haya hutegemea Aina ya BLOG na
makala zinazowekwa,Kwa mfano ni vigumu kuingiza fedha haraka
kama utafungua blog ya ktoa taarifa na habari.Hata hivyo ukiwa
Mbunifu zaidi hakutakuwa na kikwazo.
1.KUWEKA MATANGAZO YA WATU KISHA WAKAKULIPA
Hii ni njia namba moja na maarufu sana utakayoweza kuitumia
kujiingizia kipato kupitia blog yako.Fahamu kuwa kuna
wafanyabiashara ambao wanatafuta wateja mtandaoni.Ili uweze
kumshawishi mtu aweke tangazo lake katika blog yako lazima blog
yako iwe na vitu vifuatavyo:
i)Lazima blog yako iwe na watembeleaji wengi.
i)Lazima blog yako iwe hai(hii ina maana ya kwamba blog yako iwe
inawekwa makala mara kwa mara,isiwe umeweka makala leo,kisha
unakaa mwezi mzima haujaweka makala).
2.Kuifanya blog yako iwe ya kulipia
Hii ni njia ya pili unayoweza kuitumia kujiingizia kipato
kupitia.Faida kubwa iliyopo ni kwamba wewe ndiye unaamua nani
atazame blog yako.Unaweza ukaifunga blog yako na ikawa hakuna
mtu anayeweza kuingia katika blog yako bila ya wewe kumruhusu.Na
utamruhusu pale atakapofanya malipo.
KUMBUKA:Ili kuweza kutumia njia hii na uweze kufanikiwa katika
kujiingizia kipato kupitia blog yako ni lazima uandike vitu vya
thamani,yaani uandike vitu ambavyo vina faida kwa watu,pia viwe
vitu ambavyo havipatikani sehemu nyingine yoyote bure.Usihofu
sio kazi kubwa unachotakiwa kufanya ni kujifunza sifa au stadi
za blogger aliyebobea.
Blogger=Mtu anayemiliki blog au anayeandika makala katika blog
au mwendeshaji wa blog.
Jifunze jinsi ya kuwa Blogger aliyebobea(Mtaalamu).
Zifuatazo ni sifa za Blogger aliyebobea(Unatakiwa uwe nazo sifa
hizi ili uweze kujiingizia kipato kupitia Blog).Usijali sio
lazima zote,Anza na chache Nyingine Utajifunza Baadae.
i/.Uwezo wa kuandika makala zenye mvuto na zinazoeleweka.
ii/.Uwezo wa kufanya tafiti,Blogger anatakiwa awe na uwezo wa
kufanya utafiti juu ya yale anayotaka kuandika.
iii/.Blogger anatakiwa awe na uzoefu na Mitandao tafutaji(Search
Engines) .
.Blogger anatakiwa awe na ujuzi wa kuandika kiufasaha.Andika
kitu kinachoeleweka.
iv/.Kuwa na Nidhamu katika Blog yako.Weka Makala lkatika blog
yako kwa Utaratibu Maalumu.
v/.Ujuzi katika matumizi sahihi ya picha namichoro.Picha na
michoro ina umuhimu Mkubwa katika ka kuonngeza mvuto wa Makala.
.
3.Kuweka matangazo ya Google ADsense/Adword.
Unaweza kuweka Matangazo kutoka Google /Wordpress na Ukalipwa
kutokana na idadi ya watembeleaji wa blog yako watakaotembelea
Blog hiyo.Kuna sifa za kuweza kuruhusiwa kuweka Matangazo ya
Google au WordPress.
Hii pia inahitaji blog yako iwe na makala za kutosha na iwe na
watembeleaji wakutosha.
4.Kutoa kozi mbalimbali ambazo watu watakuwa tayari kujiunga
nakozi hizo NA KUZISOMA KWA MALIPO UTAKAYOWATOZA.Hii wala si
kazi kubwa ingawa inahitaji muda na kujitoa.Kama una ujuzi
wowote na unataka kuwafikishia watu kisha wakulipe basi fahamu
kuwa kupitia blog unaweza kuwafikia watu wengi sana
utaifanikisha kazi hii kupitia blog yako.Nakushauri kutumia
Kiswahili kwani ndiyo lugha ambayo watanzania wengi wana umahiri
nayo kuliko lugha nyingine.
Ili uweze kufanikisha hili unatakiwa uweke ulinzi(wa password)
KATIKA KOZI ZAKO.
5.Kutangaza biashara zako.
Tukiacha kutangaza biashara za watu pia wewe mwenyewe unaweza
kutangaza biashara zako na ukaongeza wateja kupitia blog
yako.Hii inajumuisha bidhaa zote za mtandaoni na zisizo za
mtandaoni.Unaweza kuandika vitabu mbalimbali kuanzia vya masomo
hadi vya hadithi na kadhalika.Vitabu hivi utaviandika kupitia MS
Word au program nyingine inayoweza kufanya huduma hiyo na
utawauzia wateja kwa kuwatumia katika email zao.
Ili uweze kupata soko la uaminifu unaweza ukaandika kitabu cha
kwanza na kukitoa BURE KABISA au kwa Ofa.Usishangae, kufanya
hivi kutajenga uaminifu mkubwa na kama kitabu chako kitakuwa
kizuri basi unaweza kupata soko kubwa kwa vitabu utakavyovitunga
baadae na kuviuza.
KUONGEZA WATEMBELEAJI KATIKA BLOG YAKO
1.Itangaze Blog yako katika Mitandao ya kijamii,kama vile
Facebook,Twitter,Instagram,WhatsApp na kadhalika.
2.Andika makala zenye mvuto na zinazoeleweka.Hii itawafanya
watembeleaji wawe wanatembelea mara kwa mara.
3.Itangaze blog yako kwenye mitandao mikubwa yenye watembeleaji
wengi.
4.Kuwa na utaratibu wa kukomment katika mitandao mikubwa yenye
watembeleaji wengi.kisha acha link ya blog yako,kwa njia hii
unaweza kupata watembeleaji,ila jitahidi kukomment kitu chenye
maana/thamani.
5.Chukua maoni ya wasomaji wako na uyafanyie kazi,hii itawafanya
wasomaji wako waendelee kutembelea blog yako kwani watakuwa
wanakipata wanachokitaka.Ukienda kinyume na wasomaji wako
,wanaweza kukukimbia na kutafuta blog nyingine itakayowafaa.
6.Weka makala katika blog yako kwa utaratibu maalumu.
7.Andika makala za muda mrefu.Makala za muda mrefu zina manufaa
makubwa kwani hatakama makala uliiandika mwaka uliopita bado
itakuwa na thamani.Na watu wataendelea kuisoma kwani bado ujumbe
unatumika.Makala za habari zinadumu kwa muda mfupi sana.
8.Kuwa mbunifu ifanye blog yako iwe ya kuvutia,Buni Mwonekano wa
blog yako uwe wa kuvutia,kuna rangi nyingine Ukiweka unafukuza
watembeleaji(Color Psychology).
9.Kichwa cha makala kinachovutia.
Jitahidi kuandika kighwa cha makala kinachovutia ili umshawishi
MSOMAJI Kuendelea kusoma.
10.Watambue wasomaji wa Blog yako.
Ni vema uwe na wasomaji 10 wa blog yako unaowatambua,kuliko kuwa
na wasomaji 100 usiowatambua.
Ninapozungumzia kufanikiwa kupitia BLOG yako wengi wanweza
wakapeleka mawazo yao katika UCHUMI,HASHA sina maaan hiyo,bali
ninachikusudia hapa ni jinsi gani unaweza kufanikiwa katika blog
yako.Hii ni kwa sababu watu walio wengi hawadumu katika blog zao
,yaani mtu akifungua blog baada ya muda mfupi tu miezi kadhaa(na
wengine hata siku kadhaa) HIVYO mtu wa aina hii ameshindwa
kufanikiwa katika blog yake.
Zifuatzo ni sababu zinazowafanya Watu wengi washindwe kufanikiwa
kupitia blog zao.
1.Kiwewe cha BLOG.
Nini maana ya kiwewe cha blog? Kiwewe cha Blog ni hali ya mtu
kutamani sana awe na(amiliki) blog,na kufikiria kuwa ni kazi
rahisi sana,Ukweli ni kwamba KUTENGENEZA BLOG ni kazi rahisi
sana,tatizo linakuja katika jinsi ya kuiendesha.Inahitaji
nidhamu ya hali ya juu sana la sivyo safari yako ya blog
itaishia njiani.Sababu hii huwafanya wengi waachilie mbali
kuhusu blog na hivyo kushindwa kufikia malengo.
2.UTIAJI Chumvi wa baadhi ya watu katika Matangazo yaao ya
kujinadi.
Kuna baadhi ya watu wanatia chumvi sana kiasi kwamba inaonekana
kuwa kutengeneza/kujiingizia fedha kupitia blog ni kama kazi ya
saa moja tu.Mfano unaweza ukakuta tangazo linalosomeka ‘’FUNGUA
BLOG LEO UANZE KUPOKEA FEDHA’’ au “FUNGUA BLOG LEO UANZE
KUINGIZA KIPATO CHA MAANA,SI AJABU WENGINE WANAFIKIA HATA KUSEMA
UWE TAJIRI’’.Matangazo ya namna hii na kwa mtu mwenye uelewa wa
chini anayachukulia kama yalivyo.Pia wanashindwa kufahamu kuwa
hiyo ni Lugha ya kibiashara tu.SI UONGO BLOG inaweza kukufikisha
KWENYE UTAJIRI Lakini si kwa haraka na kiurahisi namna hiyo.Watu
wa namna hii mara nyingi huishia kufunguia blog tu na kuiacha
kwani anakuta mambo tofauti na vile alivyoambiwa.
3.KUKOSA CHA KUANDIKA
Wapo wanaoshindwa kupata cha Kuandika,na hivyo huishia kati
katika safari yao ya Blog.
>>>SULUHISHO:Hakuna kitu kipya Duniani usiogope kuona hakuna
kipya,utakachoandika kwa kuona kila kitu kimeshaandikwa.Andika
tofauti na Wenzako,kuwa Mbunifu na hii ndio faida ya kufanya
utafiti kwani utafahamu mapungufu ya wengine katika makala zao
na utajua jinsi gani utayarekebisha kupitia makala zako mpya
utakazoandika.
PIA,Jijengee utaratibu wa kujisomea Soma Vitu Mbalimbali
vitakavyokuongezea Maarifa.Soma mtandaoni,soma vitabu,soma
magazeti n.k.Ukijijengea utaratibu wa kujisomea utaongeza
maarifa ya kutosha yatakayokuwezesha kupata makala za
kuandika,sio kucopy.
4.KUTOKUWA WAVUMILIVU
Kuifanya Blog yako iwe chanzo cha mapato inahitaji Muda wa
kutosha.Sio rahisi kuanza kufungua Blog leo na kesho ukaanza
kupokea fedha.Kutokana na hali hii watu wasiokuwa wavumilivu
huamua kuachana na Blog.
>>>SULUHISHO:Inahitaji kuwa Mvumilivu ili uweze kufanikiwa
katika blog yako.Kuwa Mvumilivu na tumia mbinu mbalimbali
kuiboresha blog yako.
5.KUTOPATA WATEMBELEAJI
Kupata Watembeleaji katika Blog yako inategemea vitu vingi.Kuna
watu wanapofungua blog na kuona hakuna watembeleaji huamua
kuachana na blog.
>>>>SULUHISHO:Ili kuongeza Watembeleaji katika blog yako Tumia
mbinu zifuatazo.
*UNAHITAJI USHAURI KUHUSU BLOG YAKO TUANDIKIE(BURE!!)
E-Mail:godfreymtega@gmail.com
"TUTAKUTENGENEZEA APPLICATION YA ANDROID YA BLOG YAKO"
TUNAKUTENGENEZEA BLOG KWA GHARAMA NAFUU KUANZIA TZS 10,000/= TU
TUPIGIE 0758297744
*****************************************************
Page 1 of 1