URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: <span style="color: #123aab; font-weight: bold;">Ri...
       *****************************************************
       #Post#: 3302--------------------------------------------------
       Jinsi ya kuandika habari kwenye blog ili watu waipende
   DIR By: stakeholder
       Date: October 20, 2016, 10:13 am
       ---------------------------------------------------------
       Habari za majukumu. Katika uandishi wa blog kuna vitu vya
       kuzingatia ili upate watembeleaji wengi kwenye blog yako na
       mapato yaongezeke. Usipofuata ushauri huu itafika siku utakata
       tamaa ya uandishi wa blog.
       Unapoandika chochote kwenye blog hakikisha unaweka kichwa cha
       habari yaani title ya habari yako. Tittle iendane na habari yako
       yaani iwe summary ya story nzima. Pia tittle iwe fupi mfano
       sentensi ya maneno kumi kushuka chini kama "Raisi magufuli
       amtumbua mkurugenzi wa jiji la mtakuja" Uandishi huu utakusaidia
       kupata watu wengi kupitia google yaani watu wanaosearch habari
       kwenye mitandao.
       Pili punguza kukopi habari kwenye blog nyingine na kuziweka
       kwenye blog yako. Kama umeona habari hiyo itakuletea watu wengi
       kwenye blog yako basi kopi ila hakikisha unaedit yaani ongeza
       maneno yako na futa baadhi ya maneno kuifanya iwe tofauti na
       habari uliyokopi. Ukikopi na kupaste kwenye blog unayoandika
       inawezqa kupelekea blog yako kutoweka yaani kuwa deleted hapo
       ujue utakuwa umepoteza ajira yako kwa sababu ya
       kutojishughulisha kubuni habari zako binafsai.
       Tatu hakikisha mwisho mwa habari yako unaandika jina lako kama
       kama mtunzi na mwandishi mfano "Imetayarishwa na Ana tesha"
       Endelea kutembelea jukwaa la chatguest kila siku ufundishwe
       namna ya kutajirika kupitia uandishi wa blog
       *****************************************************
       Page 1 of 1