URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Makala Bora
       *****************************************************
       #Post#: 3290--------------------------------------------------
       Unajua Madhara ya Dawa za Kusimamisha Uume Kwa Muda Mrefu?
   DIR By: ommy
       Date: October 15, 2016, 3:11 am
       ---------------------------------------------------------
       Kuna baashi ya wanaume wanatamani wakati wakiwa wanafanya
       mapenzi na wenzi au wapenzi wao basi uume zao ziwe zinasimama
       muda mrefu mathalani masaa matatu au manne au zaidi huku
       wakimwaga shahawa eti tu wawaridhishe wenzi wao au ili waonekane
       ni wanaume waliokamilika. Wanaume wengine wamekuwa wakitumia
       dawa za kusimamisha uume kama vile viagra au dawa za asili na
       zingine maarufu kama dawa za kimasai! Napenda nikwambie kwamba
       hizo dawa zina madhara makubwa kwa urijali wako na uko hatarini
       kuupoteza hata huo urijali mdogo uliosalia!
       Kusimamisha uume kwa muda mrefu na mara nyingine kiasi cha
       kufikia uume inaanza kuuma kutokana na kusimama muda mrefu
       tayari ni ugonjwa. Kwa maneno rahisi ni kwamba umetumia dawa za
       kuongeza nguvu ili kuua nguvu chache ulizokuwa nazo. Kitalaamu
       hali hiyo ya uume kusimama muda mrefu na kuuma inaitwa
       'Priapism'. Priapism hutokea pale uume inapopoteza uwezo wake wa
       kuondoa damu iliyoko kwenye uume hiyo (ambayo hufanya isimame)
       ili isinyae (in order to become flaccid). Hiyo hali ikidumu kwa
       muda wa masaa manne husababisha seli za damu iliyoko kwenye uume
       kukosa hewa ya oksijeni, hivyo kupelekea tishu katika uume kufa.
       Na kadri hali hiyo inavyoendelea hupelekea damu kwenye uume kuwa
       na asidi na hivyo kukosa uwezo wa kusafiri au kutembea kwenda
       sehemu zingine za mwili hususan kwenye moyo! Hapo hali inakuwa
       mbaya sana!
       Kuna wanaume wengine wanaji-overdose viagra au madawa ya
       kienyeji ili wawe wanaume shababi kwelikweli kumbe ndio wanaua
       uume zao. Ndio maana watu wanaotumia madawa hayo baada ya muda
       fulani hali zao za kiume zinakuwa mbaya zaidi afadhali ya jana!
       Ndio maana humu katika blog nimesisitiza sana matumizi ya
       vyakula na viungo kama tiba ya tatizo la ngivu za kiume!
       Siwashauri kutumia hayo madawa, otherwise, keep using them for
       your own risk!
       Bahati mbaya au vyovyote vile kama umesimamisha uumemasaa kadhaa
       hakikisha katika kipindi cha ndani ya masaa manne tafuta tiba
       haraka kwa daktari! Wengine baada ya kutumia hayo madawa na uume
       kusimama kama msumari masaa mengi wao hudhani dawa ni kufanya
       mapenzi masaa mengi na mwanamke ili kuondokana na hali hiyo!
       Tena wengine ndo hufurahia eti 'leo mwanamke fulani nitamfaidi
       kweli...'. My brother you are killing yourself'!!! Hutoweza
       kumkomoa mwanamke kwa kufanya mapenzi! Matibabu ya tatizo hilo
       ni kunyonya damu kwa kutumia sindano itakayochomwa kwenye mshipa
       wa damu uitwayo vein kwenye uume yako! Mwisho nakushauri kula
       sana vyakula vya asili kama matunda na mboga za majani. Usisahau
       mazoezi ya viungo.
       *****************************************************
       Page 1 of 1