URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la wanafunzi Tanzania (JUWATA)
       *****************************************************
       #Post#: 3256--------------------------------------------------
       Matokeo ya darasa la saba 2016 fuatilia hapa 
   DIR By: stakeholder
       Date: September 11, 2016, 3:50 am
       ---------------------------------------------------------
       Matokeo ya darasa la saba 2016 habari zote tunapeana hapa.
       Hongera ewe mtoto wa darasa la saba uliyehimu darasa la saba
       mwaka 2016. Nikupe pongezi nawe mlezi wa mtoto au mzazi wa mtoto
       huyu ambaye anasubiri matokeo yake sasa.
       Elimu bure tumshukuru mh Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania
       Dr john pombe Magufuli kwa kuipa kipaumbele sekta ya elimu
       Tanzania. Ndugu mzazi/ mlezi na mwalimu wa mtoto aliyehitimu
       masomo yake mwaka 2016 ninaomba mtoto huyo umuendeleze asiishie
       hapo alipofika. Dunia ya sasa inahitaji watu wenye elimu angalau
       ya sekondari. Vinginevyo mtoto huyu ataishi katika mazingira
       magumu sana. Chukulia mfano hata sekta ya kilimo ambayo zamani
       sekta hii ilikuwa inaendeshwa na watu walioshindwa kujiendeleza
       kielimu yaani mtoto akifeli anachukua jembe na kuingia shambani
       analima anapata mazao yake vizuri tu lakini sasa kilimo nacho
       kinahitaji wasomi. Zama zimebadilika kilimo kina changamoto ya
       uhitaji wa kutumia teknolojia ya kisasa ili mkulima afanikiwe.
       Sasa kwa elimu ya darasa la saba utafanya kilimo gani?
       Shule zimejengwa za kutosha kipindi cha Rais mstaafu jakaya
       mrisho kikwete wengi walimbeza kuwa shule za kata hazina viwango
       vya kutoa elimu lakini leo hii ni msaada mkubwa kwa mtanzania
       kwani kila kata ina shule walimu wapo madawati yapo japo kuna
       changamoto ambazo zinatatuliwa na serikali ya sasa kama
       kupambana na uhaba wa madawati.
       Mtoto huyu anayesubiri matokeo ya darasa la saba 2016 mwanzishie
       tuition au pre-form one ili mwakani akichaguliwa kidato cha
       kwanza asiwe mgeni sana wa masomo ya kidato cha kwanza. Wengi
       wetu ni walezi fake mtoto akihitmu masomo yake tunamwacha
       anaranda randa mitaani anashinda ana bet vijiweni na kushabikia
       mipira badala ya kumfundisha mtoto stadi za kazi na kumwandaa na
       ngazi ya elimu inayofuata. Badilika mzazi fake na mlezi fake
       wewe.
       Unajiandaaje na kumpeleka mtoto huyo kidato cha kwanza 2017?
       Kwanza kabisa nakushauri tuma maombi mapema shule za binafsi
       angalau mbili ili kama mtoto huyo atakosa nafasi shule za
       serikali basi utampeleka kwenye shule za binafsi. Endelea
       kufuatilia hapa chatgues.com kila mara ili upewe taarifa na
       majina ya watoto wa darasa la saba waliofaulu mtihani huo.
       chatguest.com inaweza kukupa taarifa hizo kwa email yako
       jisajiri dakika mbili tu ili utumiwe matokeo ya darasa la saba
       2016
       #Post#: 3306--------------------------------------------------
       Re: Matokeo ya darasa la saba 2016 fuatilia hapa 
   DIR By: stakeholder
       Date: October 28, 2016, 5:42 am
       ---------------------------------------------------------
       Tazama hapa matokeo ya mtihani wa darasa la saba 2016 bofya link
       hii
  HTML http://necta.go.tz/matokeo/2016/psle/psle.htm
       *****************************************************
       Page 1 of 1