DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
habari
HTML https://habari.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: Makala Bora
*****************************************************
#Post#: 3227--------------------------------------------------
RAIS MSTAAFU AMJIBU MWANASIASA MKONGE KINGUNGE NGOMBARI MWIRU.
DIR By: judge
Date: August 25, 2016, 4:36 am
---------------------------------------------------------
Hatimaye yale yaliyokuwa yanasubiriwa kwa hamu kutoka kwa
washabiki na wasio washabiki wa mwanasiasa mkongwe nchini Mzee
Kingunge Ngombari Mwiru yametimia jana baada ya ukimya mrefu
baada ya uchaguzi wa mwaka jana 2015 wa kuchagua Rais,Wabuge na
Madiwani ambao ulikuwa na ushindani mkubwa kati ya Mwamvuli wa
UKAWA ulioongozwa na aliyekuwa Waziri Mkuu Mstaafu Mh.Edward
N.Lowasa alipo hama kutoka chama tawala mwezi wa nane.
Uchaguzi huo ulivuma kila kona ambapo Dr.John Pombe Joseph
Magufuli alipata nafasi ya kupeperusha bendela ya chama tawala
dhidi ya mpinzani wake Edward Lowasa na hatimaye kuibuka kidedea
kumshinda Edward Lowasa na kuwa Rais wa Jamhuri ya muungano wa
Tanzania Dr.John Joseph Magufuli kwa kipindi cha miaka mitano
2015-2020.
Mwanasiasa mkongwe aliahidi kuzungumzia utendaji wa rais wa sasa
baada ya kutimiza siku mia moja za kuwa Ikulu na kuwa
madarakani, baadaye alipofuatwa mwanasiasa huyo ambaye naye
alifuata nyayo za Mh.Edward Lowasa kuzungumzia utendaji wa Rais
alisema wakati ukifika atasema anaomba wamuache.
Jana kaibuka na kuingilia mgogoro wa kisiasa ulipo sasa kati ya
maandalizi ya maandamano ya UKAWA waliyoyaita UKUTA na serikali
iliyoko madarakani,ameomba viongozi wasitaafu kuingilia swala
hilo na kumshauri rais ili kuwanusuru watanzania ambao huenda
wakaingia kwenye vita bila kutathimini madhara yatakayotokea.
Pia mwanasiasa huyo amesema kuwa Rais mstaafu wa awamu ya nne
hana sifa za kuingia kwenye kikao cha wastaafu kutokana na
kuvunja katiba kwa kutompitisha Mh.Edward Lowasa katika
kinyanganyiro cha kupata nafasi ya kupeperusha bendera ya chama
tawala CCM kwenye vikao vya kamati kuu kilichofanyika mwaka
jana.
Naye Rais Mstaafu wa awamu ya nne ambaye kwa sasa amepumzika
kwake Msoga anajibu hoja ya Mwanasiasa huyo mkongwe.
*****************************************************
Page 1 of 1