URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Makala Bora
       *****************************************************
       #Post#: 3225--------------------------------------------------
       MALEZI MUHIMU KWA MTOTO MDOGO.
   DIR By: bahati93
       Date: August 25, 2016, 2:26 am
       ---------------------------------------------------------
       Hakika kulea mtoto mchanga ni tabu sana. Kutokana na mtoto mdogo
       kuwa uwezo mkubwa wa kutambua mazingira yanayomzunguka. Hii
       inatokana na sababu milango yake ya fahamu inafanya kazi
       asilimia mia vituko vyake sasa ukijigusa kidogo tu ameshasikia
       na hivyo kustuka kutoka usingizini na yeye kutaka usingizi wake
       na hajui ataupataje itabidi alie kwasababu ndo njia pekee
       anayoijua itamfanya kupata anachohitaji kama mzazi inabidi
       uhakikishe kila atakacho mtoto wako anakipata haraka uwezavyo.
       Kwa kufanya hili utamwezesha mtoto wako uwezo wa kutambua
       kuamini katika watu ili kutatua matatizo yake hapo mbeleni
       atakapokuwa mtu mzima. So kama utakutana na mtu mkubwa ambaye
       kila kitu anataka kufanya mwenyewe haamini mawazo ya mtu
       mwingine na hashauriki jua ya kwamba hapo awali katika utoto
       wake hakutendewa wema na walezi wake hivyo basi kumfanya kukomaa
       katika kutatua matatizo yake mwenyewe.
       Mtoto mdogo huwa hajui vituvingi na hivyo katika maisha yake ya
       utotoni hutumia kujifunza vitu muhimu katika maisha kwa kadiri
       awezavyo na kwa bahati mbaya hichi pia ni kipindi ambacho
       anajifunza juu ya hisia mbalimbali katika maisha kama furaha,
       huzuni hamasa na hizi hisia akishajifunza kubadilika zinachukuwa
       mda mwingi sana ambalo linakuwa ni jukumu zito kujitua anapokuwa
       mtu mzima kama kuwa na huzuni.
       Kutokana na huku kwetu kuwa na uhaba na kutokujua siekolojia ya
       mtoto vitu vingi tunavyofanya wazazi kwa manufaa ya mtoto
       vinaweza vikawa vinamjenga mtoto kwa upande mmoja na upande
       mwingine vinambomoa. Kama ifuatavyo mtoto mdogo bado hajaweza
       kumaster vizuri control ya viungo vyake hivyo basi tegemea kama
       anakula basi atamwaga chakula kama kutembea ataenda kushoto
       kulia so kama wewe ni baba haikupasi kumkemea kwa kumtisha
       sababu hajafanya kwa makusudi ni jinsi alivyo usitake mtoto wako
       afanye vitu kama anavyofanya mtu mkubwa hivyo kukosoa kila
       analofanya mtoto wako kwa kumlinganisha na wewe au mtoto
       mwingine au dada yake au mdogo wake humfanya mtoto kukosa hamu
       ya kuishi na kujiona yeye ni mbaya hana thamani na hapo ukubwani
       usishangae kumkuta anajiuza kama kahaba au kufanya mambo mengine
       ya kujidhalilisha sana yote jua kua mtu huyu haoni dhamani yake
       tena.
       Mahitaji mhimu kwa mtoto mdogo miaka mitatu mpaka minane ni
       kupongezwa, kuonyeshwa upendo wa wazi, hivi vitu vinaonekana
       kama vidogo lakini ni vya umuhimu sana apo ukubwani. Mtoto mdogo
       huwa anapenda kila kitu anachofanya kuwa nurse, daktari,
       mwanamziki, fundi ushonaji, na fani nyingine mbalimbali bila
       kusahau kucheza sasa pale mtoto wako anapoonyesha kitu
       anachokifanya huwa anafanya kwa jitihada zote ili uone wakati
       mwingine unafanya mambo yako ya muhimu utakuta anakuja na kuanza
       kuleta usumbufu kwa mtizamo wako lakini sio hivyo kwa mtizamo
       wake yeye anataka hongera zake na endapo hatazipata basi ndio
       mwanzo wake kukosa kujiamini katika mambo anayofanya hapo
       mbeleni kwani atakuwa hajui juu ya kujaribu na kupongezwa mtu
       unajisikiaje atakuwa anaogopa kufanya. Bahati mbaya ipo kwa wale
       watoto wanaofanya juu chini kubakia number moja darasani kwao na
       wazazi wao kuona ni kitu cha kawaida na hivyo basi wao kukosa
       uhusiano wa karibu na wazazi wao katika mafanikio yao na
       malipizi yao huwa ingawa hawajakusudia hapo ukubwani
       watakapokuwa na pesa zao hawataangaika kushare pamoja na wazazi
       wao kwa sababu hawajui waanzie wapi hicho kitu hakipo kabisa
       katika mawazo yao sasa ukaona mtu tajiri afu ukamtukana kwa
       kusema anajijali mwenyewe na kusahau wazazi wake basi hujui
       aliyopitia ili kufika hapo alipo sasa.
       Pia katika miaka hii chini ya nane mtoto huanza kujifunza juu ya
       upendo na huwa wanauelewa mkubwa kuliko wazazi tunavyozania
       mfano anaweza kuona na kutamani mdoli au gari alilonunuliwa
       mwenzake na wazazi wake na yeye atakuwa anafikiria kama kweli
       mnampenda na kumjali basi mtamnunulia na yeye. Anaweza kusema au
       kutosema kama asiposema kwa kutumia ukubwa wetu utaweza kuona
       kitu ambacho mtoto wako anakipenda na kuhakikisha unamfanikishia
       endapo ataomba na kupuuziwa basi utakuwa mtu wa kwanza kumtupa
       mkono wakati anataka uhitaji wako sana. Hili ndio huwa tatizo
       kubwa sana kama mtoto akakosa huenda hapo baadae akawa mtu
       mwenye roho mbaya sana kwa kutokujua upendo unanogaje unakuta
       mtu kuwa na wenzi Zaidi ya mmoja hii ni kutokana na  yeye kutaka
       kupata upendo ambao hapo mwanzo hakuweza kuupata kabisa na
       tambua kuwa upendo ni njia mbili nipe nikupe endapo mtoto mdogo
       akakosa upendo basi huenda hata akawa hana mwenza au kuachika au
       kuachwa kila wakati kwa sababu hawezi kupenda na kupendwa. mtu
       anajifunza haya mambo akiwa mdogo ndo basi tena usishangae kuona
       mtu mzima bado hajaowa au hana watoto chanzo ni utotoni.
       Endapo ni mmoja wapo wa wahanga wa kunyimwa malezi bora utotoni
       cha kufanya ni kuamini unaweza kuepuka mitego ya akili hiyo  kwa
       kujijengea mazoea ambayo yatajibadili kama tabia tambua mawazo
       ambayo yanakuajia kukuongoza kwenye njia mbaya na pia unaweza
       mwambia mwenza wako juu ya matendo yako mabaya ambayo anatakiwa
       kuyajua na kushirikiana kuyatatua.
       Watu ambao wamefunga ndoa walioanzisha familia na ambao wapo
       kwenye mahusiano kaeni mkipanga na kujiandaa kumkaribisha mtoto
       wenu kuhakisha mnampatia kila jambo ambalo ni muhimu kwake hivyo
       kuja kuwa mtu mzuri hapo ukubwani mwenye mafanikio ambayo
       mtakula wote na hii ndio maana kamili ya kuwekeza kwa mtoto
       wako. Na kama una watoto Zaidi ya mmoja hakikisha kutokuonnyesha
       upendeleo wala kuwalinganisha watoto wako kwamba yupi ni bora
       kuliko wenzake. Na ndo kama unaanza na mmoja basi panga uzazi wa
       mpango kuhakisha watoto wote wanapata uangalizi wa kutoshoa
       wakiwa uchangani kama unaweza kulea vichanga Zaidi ya kimoja
       usijali wewe fyatua tuu. Weka bajeti ya midoli na nguo kwa
       watotoyo wenu.
       *****************************************************
       Page 1 of 1