URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: <span style="color: #123aab; font-weight: bold;">Ri...
       *****************************************************
       #Post#: 2965--------------------------------------------------
       seebait.com ni mkombozi kwa bloggers wa tanzania
   DIR By: master
       Date: February 26, 2016, 1:36 pm
       ---------------------------------------------------------
       Tanzania tumepata mtandao wa kupokea na kuweka matangazo seebait
       ad network mtandao huu hakika unalipa vizuri kuliko hata google
       adsense. Kwa waliojiunga na google adsense nadhani wanakubaliana
       na mimi kuwa adsense ndiyo mtandao pekee duniani uliokuwa
       unalipa bloggers vizuri. wengine ni wababaishaji tu.
       Lakini google adsense bado haikuwa mkombozi wa Tanzania bloggers
       kama ilivyo sasa kwa hawa seebait. Sababu ni kwamba google
       adsense inawalipa vizuri wanabloggers wanaotumia lugha ya
       kingereza kwani keywords zao ndiyo zinazonunuliwa kwa gharama
       kubwa kuliko keywords za kiswahili. click ya tanzania ina bei
       ndogo ukilinganisha na click ya marekani au kenya. Huu ulikuwa
       ubaguzi mkubwa kwa wamiliki wa blog.
       Sasa kilio cha bloggers kupata mtandao mzuri wa kupokea
       matangazo kimekwisha. seebait imekuja kipekee. inakulipa 1850
       kwa kila 1000 impressions hii ni bei nzuri kwa bloggers
       ukilinganisha na google adsense inayolipa hado 0.09 kwa 1000
       impressions pesa ndogo sana.
       Ushauri bloggers wekeni malengo ya kuzifanya blog zenu kuwa
       ajira. facebook ilianza kiutani utani lakini leo inatengeneza
       mabilioni ya pesa kwa mwezi. Hata wewe unaweza kuwa tajiri kwa
       kujiajiri kupitia blog yako hiyo unayoiendesha kwa faida ya
       kujulikana na watu tu bila kuwa na malengo ya kupata pesa nzuri
       kupitia blog yako hata uweze kununua gari zuri kutokana na pesa
       unazopata toka kwenye blog hiyo. Hakikisha unaandika story za
       kuvutia watu kwenye blog yako ili upate wafuasi wengi
       watakaoitangaza blog yako huko mitaani hatimaye utajikuta
       unapokea watu zaidi ya elfu kumi kwa siku na kutengeneza si
       chini ya elfu hamsini kwa siku moja kupitia matangazo.
       Pia ushauri kwa kampuni ya seebait endeleeni kusaidia bloggers
       wafikie malengo kwa kuingia mikataba na makampuni makubwa kama
       vodacom airtel tigo wawe wanatangaza kwenye mtandao wa seebait
       ili bloggers nao wanufaike pale makampuni haya yanapoweka
       matangazo kwenye blogs hizi. Wote tunajua ni ngumu sana kwa
       blogger moja anayepata watu miamoja kwa siku kupata matangazo
       yatakayomlipa kwenye blog yake lakini kupitia mawakala wa
       matangazo kama seebait google adsense au infolinks hata blogger
       ambaye kwa siku anapata watazamaji 50 ataweza kuweka matangazo
       kwenye blog yake na atapata vijisenti hata vya kununulia mb data
       za kumuwezesha kujiunga na internet kila siku na kufanya kazi
       yake ya blogging
       Kama bado hujajisajiri na see bait basi jisajiri leo upige pesa
       kwenye blog yako
       *****************************************************
       Page 1 of 1