URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la elimu Tanzania
       *****************************************************
       #Post#: 2828--------------------------------------------------
       ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za walimu
       2016
   DIR By: mastory
       Date: February 16, 2016, 3:30 am
       ---------------------------------------------------------
       "
  HTML https://3.bp.blogspot.com/-bA6bs0ucc_s/VsLSNGbc5HI/AAAAAAAABBY/a6ozrs-ZLmk/s400/Jaffo-16Feb2016.png
       Serikali inatarajia kutoa ajira 40,000 kwa walimu wa shule za
       msingi na sekondari mwaka huu.
       Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali
       za Mitaa (Tamisemi), Suleiman Jaffo, alilieleza Nipashe jana
       kuwa idadi hiyo inalenga kupunguza upungufu wa walimu shuleni.
       Jaffo alisema ajira hizo zitatangazwa mapema mwaka huu na
       zitaongeza nguvu kwenye shule zenye uhitaji wa walimu hasa mpya
       na zile zilizoandikisha wanafunzi wengi wa darasa la kwanza na
       kidato cha kwanza.
       Sambamba na hilo, ameahidi kushirikiana na Halmashauri ya
       Manispaa ya Temeke kuwezesha wanafunzi zaidi ya 5,800 wa Shule
       ya Msingi Majimatitu wanapata elimu bora.
       Alisema idadi hiyo ya wananfunzi ni sawa na idadi ya shule sita
       za msingi, hivyo itagawanywa katika shule za jirani pamoja na
       kujenga madarasa mapya katika shule hiyo.
       “Ongezeko hili la wanafunzi waliojiandikisha darasa la kwanza
       mwaka huu limetokana na mfumo wa serikali kutoa elimu bure na
       lengo la serikali ni kutoa elimu bora, hivyo kama serikali
       tutahakikisha tunaboresha mazingira kwa kuweka madawati ya
       kutosha, madarasa na walimu, hivyo hakuna mwanafunzi atakayekaa
       chini kuanzia mwezi wa sita,” alisema Jaffo.
       Pia alisema serikali itahakikisha inaongeza majengo katika shule
       hiyo pamoja na kujenga shule mpya umbali wa kilomita moja kutoka
       shule hiyo ilipo, katika kiwanja kilichotolewa na Katibu Mkuu
       Kiongozi mstaafu, Balozi Martin Lumbanga, kwa ajili ya kujenga
       shule mpya.
       Alimtaka Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Photidas Kagimbo,
       kuangalia uwezekano wa kujenga jengo la ghorofa katika kiwanja
       hicho ili kukidhi mfumuko wa wanafunzi wanaoandikishwa kila
       mwaka pamoja na kupunguzia wanafunzi wa Shule ya Mbagala
       Majimatitu katika shule hiyo mpya.
       Pia aliwataka kuwashirikisha wamiliki wa viwanda wa manispaa
       hiyo, mchakato wa ujenzi wa madarasa ili kukamilisha kazi hiyo
       kwa wakati.
       Jafo pia alimtaka Ofisa Elimu wa wilaya hiyo, Angel Frank,
       kuhakikisha walimu wa shule hiyo wanaotakiwa kupandishwa daraja
       wanafanyiwa hivyo pamoja na kulipwa mishahara stahiki kwa wakati
       kutokana na kazi kubwa wanayoifanya ya kulea watoto hao.
       Naye Mkuu wa shule hiyo, Abdallah Ngomi, alisema shule  ina
       zaidi ya wanafunzi 5,800, walimu 77 wakati mahitaji yakiwa ni
       walimu 131 na madawati 900 hali inayowalazimu kuweka madawati 52
       katika darasa moja badala ya 15 huku mahitaji ya  kwa shule
       nzima yakiwa ni 1,959.
       “Tuna uhitaji wa vyumba vya madarasa 131 na kwa sasa tunavyo 22
       pekee na tunatarajia kujenga 10, hivyo mahitaji ni 109, matundu
       ya vyoo pia tunahitaji 203 wakati tunayo 36 tu.
       "Kutokana na idadi hiyo kubwa, wanafunzi wanalazimika kusomea
       nje na wengine kuingia kwa awamu,” alisema.
       Mwaka huu shule hiyo imeandikisha wanafunzi 1,022 wa darasa la
       kwanza idadi ambayo ni sawa na wanafunzi wa shule moja."
       chanzo nipashe
       Jisajiri hapa chatguest kupitia link yangu hapo chini ili nikupe
       taarifa kwenye email yako siku wakitangaza post za ualimu 2016
       #Post#: 2835--------------------------------------------------
       Re: ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za
       walimu 2016
   DIR By: Wilson John
       Date: February 16, 2016, 8:11 am
       ---------------------------------------------------------
       Wafanye haraka katika kuajiri walimu maana hali si nzuri kwa
       shule zetu waache kuwaweka pia vijana mda mrefu kitaa.
       #Post#: 2949--------------------------------------------------
       Re: ajira za walimu 2016 soma hapa habari mpya kuhusu post za
       walimu 2016
   DIR By: moses nyingi
       Date: February 20, 2016, 1:06 pm
       ---------------------------------------------------------
       lini serikali itaajili walimu maana shule zetu zimelemewa kwa
       kuwa na wanafunzi wengi kupita uwezo
       *****************************************************
       Page 1 of 1