URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: <span style="color: #123aab; font-weight: bold;">Ri...
       *****************************************************
       #Post#: 2523--------------------------------------------------
       Blog yako ina miaka mingapi toka uifungue na imekuingizia kipato
       kiasi gani?
   DIR By: master
       Date: November 12, 2015, 11:48 am
       ---------------------------------------------------------
       Naanzisha mada hii mahususi kwa wamiliki wa blogs. Siku hizi
       blog ni chombo cha habari kama tv radio au magazeti. Huwezi
       kushangaa unapoona habari inayotangazwa ITV au TBc1 ulishaiona
       mapema kwenye blog. mfano ajari iliyotokea kijijini kusiko na
       mawakala au waandishi wa habari wa tv wala redio ni rahisi
       kuipata kwenye blog ya mtu binafsi yoyote yule aliyekuwepo
       kwenye tukio na anasimu yenye uwezo wa kuchukua picha nzuri na
       kuiweka kwenye blog yake.huu ndiyo umuhimu wa blogs kwa wakati
       huu. sasa kutokana na umuhimu wake wewe blogger umetambua kuwa
       una chombo cha habari ambacho unaweza kujiajiri wewe na
       ukawatengenezea wengine ajira? unafanya jitihada gani kuiwezesha
       blog yako ikuingizie mamilioni ya pesa kwa mwezi? karibu
       tujadili na tuongezeane ujuzi  kuhusu jinsi tunavyoweza
       kufanikiwa kimaisha kwa uanzishaji blog zenye manufaa kwa jamii
       yetu. sikuhizi watu wanatafuta habari na kutatua matatizo yao
       kupitia tovuti.
       *****************************************************
       Page 1 of 1