DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
habari
HTML https://habari.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: <span style="color: #123aab; font-weight: bold;">Ma...
*****************************************************
#Post#: 1885--------------------------------------------------
UTUNDU NA UBUNIFU HUJENGA AU HUBOA UNAPOKOSEKANA
DIR By: The Marvel
Date: July 2, 2015, 5:02 pm
---------------------------------------------------------
WAPO wanaojuta kupenda lakini mbaya zaidi wapo wanaolia kwa
sababu ya vitu vidogo vidogo ambavyo vimekuwa haviwaendei sawa
katika uhusiano wao. Ni jambo lililo wazi kwamba, usaliti
umekuwa ukiwatesa wengi tena ukijaribu kuchunguza sababu za
baadhi ya watu kuwasaliti wapenzi wao, kutoyajua mapenzi yale ya
faragha ni moja wapo.
Wapo wasichana au niseme wanawake ambao kimaumbile wana mvuto
sana. Wamejaaliwa uzuri wa sura na kila kitu kiasi cha
kutamaniwa na kila mwanaume wanayekutana naye.
Lakini linapozungumziwa suala la mapenzi kwa mwanamke, wanaume
wanaangalia vitu vingi, achilia mbali hilo la muonenako, pia
wanaangalia utundu na ubunifu wa faragha. Hapo ndipo
panapowakosesha raha baadhi ya wanawake wazuri.
Wanakuwa ni wenye kupata bahati ya kupendwa lakini hao hao ndiyo
wale ambao kila siku wanaachwa. Si jambo la ajabu huko mtaani
kukutana na msichana mkali ile mbaya lakini akawa si mtu wa
kutulia na mwanaume kwa muda mrefu, kwanini? Kwa sababu hayajui
mapenzi.
Ni tatizo siriasi ?.
Msichana mzuri aliyeumbika kutoyajua majamboz ni tatizo na ndiyo
maana anaweza kuwa mtu wa kulia kila siku.
Anaweza kukumbana na malalamiko kutoka kwa mpenzi wake kwamba
anachokipata ni tofauti na alivyotarajia. Hakuna kinachowauma
walio wengi kama kusikia kutoka kwa wapenzi wao kuwa
hawawaridhishi.
Kwa maana hiyo ni tatizo siriasi lakini lina ufumbuzi wake.
Hakuna aliyezaliwa na kuanza kutembea moja kwa moja, vile vile
kuingia kwenye uhusiano ukawa hujui lolote siyo tatizo ila
unachotakiwa kukifanya ni kujifunza.
Zungumza na wataalam wa masuala ya mapenzi, soma vijarida na
magazeti, naamini utapata elimu tosha ya kuweza kumfanyia mpenzi
wako yale yatakayomfurahisha.
Ugoigoi faragha kwa mwanamke ni chanzo cha wengi kusatiliwa,
tena utasalitiwa zaidi kama kila siku utakuwa ni mtu yule yule,
yaani hujifunzi chochote. Mwanamke lazima awe mbunifu kwa mpenzi
wake, abuni mbinu za kumdatisha ili kuhakikisha haachwi
kirahisi.
Unapobaki kujisifia kuwa wewe ni mzuri wakati huna mashamsham
yoyote itakuwa ni kazi bure. Matokeo yake sasa utashangaa mpenzi
wako anakwenda kwa mwingine ambaye ukimuangalia na
kujilinganisha na wewe, unaanza kujiuliza, hivi alichokifuata
kwa yule ni nini ?.
Hakuna kingine, kafuata majamboz. Ndiyo maana nikasema, uzuri
wako kama hujui chochote faragha, ujiandae kusalitiwa kila siku
na mwisho wake utaachwa.
Ni majamboz tu ?.
Sifa za mwanamke anayeweza kutulia kwenye uhusiano ukiachilia
mbali uzuri wa sura na umbo, tabia njema nalo ni jambo la
msingi. Kama umzuri, unayajua mambo ya chumbani ile mbaya ila
huna tabia njema, ni tatizo. Waswahili wanasema, tabia njema ni
silaha.
Ushauri wangu
Ili uyafurahie maisha yako ya kimapenzi, hakikisha unakuwa imara
kila idara. Kwanza mpende mpenzi wako kwa maana halisi ya
kumpenda halafu jitahidi kumpatia furaha ya kweli.
Miongoni mwa mambo yanayoweza kumfurahisha mpenzi wako ni
kumshibisha pale mnapopeana chakula cha usiku, ale ashibe na
wewe ushibe, mtadumu.
Mbinu za kumshibisha mpenzi wako, zipo nyingi jifunze na
zifanyie kazi
*****************************************************
Page 1 of 1