URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       habari
  HTML https://habari.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: Jukwaa la elimu Tanzania
       *****************************************************
       #Post#: 1558--------------------------------------------------
       MATAPELI, AJIRA YA WALIMU WAPYA WA SHULE ZA MSINGI, SEKONDARI NA
       VYUO VYA UALIMU
   DIR By: Nadia
       Date: March 24, 2015, 10:36 am
       ---------------------------------------------------------
  HTML http://1.bp.blogspot.com/-kZnCNajG5-w/VREpMoJ19tI/AAAAAAAARyw/7gYhcFvHDiE/s800/AA1.jpg
       JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
       WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
       TAARIFA KWA UMMA KUHUSU AJIRA YA WALIMU WAPYA WA SHULE ZA
       MSINGI, SEKONDARI NA VYUO VYA UALIMU MWAKA 2015/16
       JIHADHARI NA MATAPELI
       Kumekuwepo na Tangazo la upotoshaji kuhusu Ajira ya walimu wapya
       kwa mwaka 2015/16 (TANGAZO No. T.022/15TMS 2015) linalodaiwa
       kuwa limetolewa na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi na
       kusambazwa kwenye Mitandao ya Kijamii.
       Taarifa zilizotolewa katika tangazo hilo siyo za kweli na Wizara
       haihusiki nazo.
       Aidha, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi inapenda
       kuufahamisha umma kuwa ajira ya Walimu wa ngazi ya Cheti,
       Stashahada, na Shahada hufanywa na Ofisi ya Waziri Mkuu -
       TAMISEMI baada ya kupata kibali cha Ajira kutoka Ofisi ya Rais -
       Menejimenti ya Utumishi wa Umma. Hivyo Wizara ya Elimu na
       Mafunzo ya Ufundi haihusiki moja kwa moja na zoezi hilo.
       Kutokana na mgawanyo wa majukumu ya Wizara mbalimbali, taarifa
       sahihi kuhusu ajira mpya za walimu kwa mwaka huu wa fedha
       zitatangazwa na Mamlaka inayohusika yaani Ofisi ya Waziri Mkuu -
       TAMISEMI mara watakapokamilisha taratibu zinazotakiwa.
       Imetolewa na:
       Katibu Mkuu,
       WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI
       24 March 2015"
       *****************************************************
       Page 1 of 1