URI:
   DIR Return Create A Forum - Home
       ---------------------------------------------------------
       BongoTv
  HTML https://bongotvuserforum.createaforum.com
       ---------------------------------------------------------
       *****************************************************
   DIR Return to: International Forum
       *****************************************************
       #Post#: 6--------------------------------------------------
       Obama ajutia makosa ya Marekani nchini Libya
   DIR By: admin
       Date: April 11, 2016, 8:28 am
       ---------------------------------------------------------
       Rais wa Marekani Barack Obama amekiri kwa mara ya kwanza kwamba
       serikali yake ilifeli katika kutatua mzozo wa Libya.
       Amesema hilo huenda ndilo “kosa kubwa” zaidi alilolitenda wakati
       wa utawala wake.
       Bw Obama amesema Marekani haikua na mpango mahususi wa jinsi
       taifa hilo litakavyotawaliwa baada ya kuondolewa madarakani kwa
       Kanali Muammar Gaddafi.
       Alisema haya katika mahojiano na runinga ya Fox News kuangazia
       mafanikio na mapungufu ya utawala wake.  Hata hivyo ametetea
       hatua ya kuingilia kijeshi nchini Libya. Marekani na Muungano wa
       NATO zilitekeleza mashambulio ya anga kuwalinda raia baada ya
       kuzuka maasi dhidi ya Muammar Gaddafi mwaka 2011.
       Lakini baada ya mauaji ya kiongozi huyo, Libya ilitumbukia
       katika vita vya wenyewe kwa wenyewe kati ya makundi ya waasi
       huku makundi mawili yakiunda serikali na mabunge tofauti.
       Katika hatua za kurejesha utulivu serikali ya muungano wa
       kitaifa inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imewasili katika
       mji mkuu Tripoli ili kuanza mipango ya kuongoza nchi ya
       kurejesha hali ya kawaida.
       Uchaguzi mkuu nchini Marekani utafanyika Novemba na Rais Obama
       atakabidhi madaraka kwa mrithi wake Januari mwakani baada ya
       kuongoza kwa mihula miwili.
       *****************************************************
       Page 1 of 1