DIR Return Create A Forum - Home
---------------------------------------------------------
BongoTv
HTML https://bongotvuserforum.createaforum.com
---------------------------------------------------------
*****************************************************
DIR Return to: News & Events
*****************************************************
#Post#: 5--------------------------------------------------
Watumishi hewa wamponza mkuu wa mkoa
DIR By: admin
Date: April 11, 2016, 8:27 am
---------------------------------------------------------
Rais wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa
mkuu wa mkoa wa Shinyanga kutokana na kuwepo kwa watumishi hewa.
Bi Anna Kilango Malecela alitangaza kwenye vyombo vya habari
kuwa mkoa wake hakuwa na watumishi hewa.
Ikulu hata hivyo ilifanya uchunguzi wake na kubaini kuwepo kwa
wafanyakazi hewa 45 katika awamu ya kwanza.
Awamu ya pili ya uchunguzi huo bado inaendelea.
Akiongea Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Magufuli amesema
amesikitishwa na hali hiyo na kuagiza mkuu huyo wa mkoa na
Katibu Tawala wa Mkoa kuondolewa kazini mara moja.
Kwa jumla, zaidi ya wafanyakazi hewa 2,000 waligunduliwa baada
ya utathmini kufanywa mikoani.
source: BBC
*****************************************************
Page 1 of 1